Wednesday, March 5, 2014

12:20 AM
MSANII wa kike anayetesa kwenye Bongo Fleva, Esterlina Sanga ‘Linah’ ametoa mpya baada ya kuibuka na kueleza wazi kuwa, awapo faragha hapendi kutumia kinga.
Linah alisema hayo wakati akizungumza na mwakilishi wa kona hii jijini Dar es Salaam wikiendi iliyopita, ambapo alisisitiza kuwa anachukia sana mipira ya kike na kiume wakati wa tendo kwa vile zinamkata stimu.
“Sema naogopa ukimwi na magonjwa mengine ndiyo maana nalazimika kutumia kwa ajili ya afya yangu lakini kiukweli kabisa, sipendi kabisa kinga,” alisema Linah.
Esterlina Sanga ‘Linah’.
Hivi karibuni,  habari ya staa huyo wa muziki kudungwa mimba na mdosi kabla ya siku chache baadaye kugundulika kuwa, kiumbe chake kilichoropoka.

0 comments:

Post a Comment