Sunday, March 2, 2014

9:13 PM
Usiku wa kuamkia February 26 uliingia kwenye headline kwenye mitandao ya kijamii na hii ni baada ya kusambaa kwa video na picha zinazomuonyesha Pancras Ndaki Charles au Pnc kupiga magoti mbele ya Ostaz Juma Namusoma kama kumuomba msamaha wa kurudi kwenye kundi.Picha hizo zimeibua mambo mengi sana na baadhi ya wasanii na wadau wakubwa wakidai kuwa Ostaz Juma Namusoma kamdharirisha Pnc,miongoni mwa wasanii walioonekana kukerwa zaidi na kitendo hicho ni pamoja na member wa zamani wa kundi hilo Kitale na wadau wengine kama Adam  Juma,Suma Mnazaleth,Said Fela na wengine wengi.


Hii ni nafasi naomba tuitumie kumsikiliza Pnc mwenyewe akielezea hali hiyo>>’‘Kuomba samahani hiki kitu sijaona kama ni kitu kibaya kwangu hata kupiga goti kumuomba samahani- kwa sababu hata baba yangu siku zote nilipokuwa nikimkosea yaani ilikua kawaida yangu,baba bana nisamehe yaani kwa kwa upande wetu ni heshima tu nimechukulia’

‘Kwa sababu  mwenyewe anadai yeye hajazijichapisha yeye zile picha,tulikuwa wengi kifupi sijajua siwezi kumlaumu nikasema ostaz umechapisha inshu zangu, kikubwa kuhusu haya mambo mi napotezea naangalia mambo yangu’
‘Unajua ostaz wanamchukulia kama kaka yangu wakinipigia simu ndugu zangu wananilaumu wewe umemfanya nini ostaz,tumeshaongea na ostaz kinachofuata sasa hivi ni kuingia studio na kufanya kazi zangu kama kawaida’.

0 comments:

Post a Comment