Tuesday, March 4, 2014

1:20 AM

Wiki iliyopita muigizaji wa filamu nchini Kajala Masanja alikiri kuwekewa sumu wakati alipokuwa kwenye show ya mwanamuziki Izzo Buzness. Star huyo aliwahi hospitalini na hali yake kuwa nzuri. Hata hivyo star mmoja wa filamu akizungumza na Swahiliworldplanet kwa sharti la kutoandikwa jina lake alisema kuwa Kajala alifanyiwa kitendo hicho cha kifedhuli kutokana na madai ya kutembea na mume wa mtu ambaye anadaiwa kumpangishia nyumba ya kifahari “kachukua mume wa mtu huyo Kajala, yes kuna libaba limempangia nyumba nzima so nahisi ndiyo sababu ya kuwekewa sumu” kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo Kajala alijaribu kutafutwa ili kutolea ufafanuzi madai hayo lakini kwa siku mbili hakuweza kupatikana.

 

0 comments:

Post a Comment