Saturday, March 8, 2014

11:59 PM
1


                                                            Vincent Kigosi ‘Ray’ akiwa na mkewe mtarajiwa, Chuchu Hans.
Kwa mujibu wa sosi aliye karibu na mastaa hao (jina tunalo), Ray amemwaga shilingi milioni 3,840,000 kwa ajili ya kodi ya nyumba hiyo iliyopo Mwananyamala-Msisiri B jijini Dar es Salaam.
“Wakati wanakwenda kuiona nyumba hiyo kwa mara ya kwanza, ndani ilikuwa imezeeka lakini Ray aliamua kumwaga fedha kwa ajili ya ukarabati na sasa inaonekana ni ya kifahari tena mpya, hata wewe (mwandishi) ukiingia utasema inafaa kukaliwa na staa,” alisema sosi huyo.

Nyumba aliyopangishiwa Chuchu na mumewe mtarajiwa, Ray Kigosi.
MILIONI 1,500,000 UKARABATI PEKEE
Taarifa zaidi zimejianika kwamba, staa huyo alitumia kiasi cha shilingi milioni 1,500,000 kwa ajili ya kufanyia ukarabati nyumba hiyo, kama vile kupaka rangi, kuweka dari mpya, kurekebisha milango sanjari na vitasa, kubandika marumaru na mambo mengine kibao ya kuinakshi, hali iliyowashtua watu wengi.
Nyumba hiyo inadaiwa ina vyumba vitatu vya kulala, sebuleni kubwa, jiko, bafu, choo, stoo na ua mkubwa wa kulaza magari kadhaa (kama anayo).
MASTAA WAMSHANGAA RAY
Wakati staa huyo akidaiwa kuwajibika kwa staili hiyo kwa mpenzi wake huyo, baadhi ya mastaa waliozungumza na gazeti hili walifungukia wakikikejeli kitendo hicho.



Paparazi wa GPL akiongea na hausigeli wa Chuchu.
“Hivi huyu jamaa (Ray) ana akili kweli? Au ndiyo huko kupenda? Anashindwa kuimalizia nyumba yake kule Mbezi (hakusema Mbezi ipi), anabaki kutengeneza nyumba ya watu huku akilipia kodi kubwa,”alisema staa mmoja huku akiomba chondechonde jina lake lisichorwe gazetini.
WAANDISHI MTAANI
Baada ya kuzinyaka habari hizo, waandishi wetu walijitosa mtaani kuisaka nyumba hiyo katika maeneo yaliyotajwa ya Msisiri.
CHUCHU HANS NDANI YA BAJAJ
Makadirio ya kiasi cha mita hamsini kufika kwenye nyumba hiyo, Chuchu Hans alitoka na kuingia ndani ya Bajaj yenye rangi nyekundu (namba za usajili hazikupatikana) na kuelekea kusikojulikana.


Mainda.
MAPAPARAZI WAIBAINI NYUMBA
Baada ya Chuchu kuishia, mapaparazi walibaini kuwa nyumba hiyo ndiyo ambayo Ray amejitutumua na kumpangia mrembo huyo.
Nje ya geti jeusi, waandishi walibisha hodi, akatokea msichana aliyejitambulisha ni msaidizi wa kazi za ndani katika nyumba hiyo, yaani ‘hausigeli’.
Paparazi: Tumemkuta Chuchu Hans?
Hausigeli: Hapana. Ametoka sasa hivi.
Paparazi: Amekwenda wapi?
Hausigeli: Mi sijui.
Paparazi: Hakuna mtu mwingine mkubwa mwenye kuweza kuzungumza na sisi chochote?
Hausigeli: Hakuna.
Paparazi: Haya, asante!
Hausigeli: Haya, karibuni.


Johari.
CHUCHU KWENYE SIMU YA MKONONI
Baadaye, Amani lilimpigia simu Chuchu kwa lengo la kutaka kumsikia alichonacho kuhusu nyumba hiyo, lakini simu  hiyo ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
MSIKIE RAY
Kutokana na maadili ya taaluma ya habari, madai hayo ilikuwa lazima pia yamfikie Ray ambaye ndiye anayedaiwa kuonesha jeuri ya fedha.
Paparazi: Mambo Ray?
Ray: Poa, mzima?
Paparazi: Mi mzima tu.
Paparazi: Ee bwana, hapa ni Global Publishers, kuna ishu nataka kujua. Tumepokea habari kwamba umempangia nyumba Chuchu pale maeneo ya Mwananyamala Msisiri. Labda tuanzie hapo, ni kweli madai hayo?
 Ray: No comment (akakata simu).


Nyumbani kwa Chuchu.
JOHARI AZIDI KUKONDA
Vuguvugu la Ray na Chuchu kuwa wapenzi, kumesababisha kuharibu mfumo wa maisha ya watu waliodaiwa tangu zamani kwamba ni wapenzi wake, Blandina Chagula ‘Johari’ na Ruth Suka ‘Mainda’.
Kuzidi kupungua uzito kwa Johari kunatajwa kuwa chanzo ni Ray kummwaga yeye na kuhamishia kambi kwa mwanadada huyo. Amewahi kuulizwa kuhusu hilo lakini amekuwa mgumu wa kusema ukweli licha ya kwamba za chini ya kapeti kwa mastaa zinakiri hilo.
Kwa upande wake, Mainda alipoulizwa na Amani kuhusu anavyojisikia Ray kuwa na Chuchu alifunguka yote (yaliandikwa kwenye Gazeti la Risasi Mchanganyiko). Lakini mwisho wa maneno yake yote ni kumwachia Mungu na kwamba, ameshaamua kuishi kivyake akimwona ‘zilipendwa’ huyo kama alimpotezea muda.
credit : GPL

1 comments: