Sunday, March 9, 2014

12:04 AM
Mkiambiwa michepuko sio dili nyie mnakomaa mnajiona vidume kuwa na warembo wengi.. katika hali ambayo iliwashangaa watu wengi na kuwaacha midomo wazi wakazi wa mji wa kigamboni ni pale jamaa mmoja sharobaro mzuri tu alipochezea kichapo baada yakugonganisha magari,, hapa wanaume viwembe mnaelewa naposema kugonganisha magari..


Inasemekana jamaa huyo anasoma chuo kimoja hapa town na amekuwa na tabia ya kuwadump watoto wa kike.. shehuda wa tukio hilo wanasema jamaa huyo aliingia katika nyumba yake ambapo amepanga na wakati anaigia aliongozana na msichana mwembamba hivi.. na baada ya masaa kama mawili alikuja dada ambaye alipakizwa kwenye bodaboda na ndipo alipogonga na kufunguliwa mlango.. baada ya hapo watu walisikia malumbano huko ndani mara pakawa kimya na ndipo jamaa alipotoka akiwakimbiza mabinti hao huku akivuja damu mdomoni na puani  jambo lililohashiria kuwa jamaa alipewa kichapo toka kwa wadada hao,,,  hii nadhani ni fundisho kwa wengi wetu, achana na michepuko la sivyo kama sio kukwaa ngoma huko maangaikoni yatakukuta ya huyu jamaa....

0 comments:

Post a Comment