Wednesday, December 4, 2013

11:29 AM


  Mzee Tulito akiwa kwenye gari tayari kupelekwa hospitali
Mzee huyu wa jamii ya kabila la wamasai aliyetambulika kwa jina la ''Tulito'' Mkaazi wa KIA njia panda ya kuelekea uwanja wa ndege wa Kilimanjaro International Airpot, Leo mda mfupi uliopita amepata ajali mbaya ya kugongwa na fuso alipofanya jaribio la kuvuka barabara hio ya lami ambayo magari huenda mwendo kasi, Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka mkoni kilimanjaro kimedai kwamba gari hilo aina ya FUSO halikusimama baada ya kumgonja mzee Tulito lilitokomea..! Raia waliokuwa karibu na eneo la tukio hawakufanikiwa kunasa walau hata namba za gari hilo, Mzee tulito aliwahishwa Hospitali wilayani boma kwa matibabu zaidi.
Imeripotiwa na Afande wa Ust taifa (Dj Tindo)
Picha zaidi............
Majeruhi huyo akiwa amelala huku mashuhuda wa tukio hilo wakimtazama





0 comments:

Post a Comment