Thursday, February 27, 2014

1:29 PM
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), ameendelea kuweka pingamizi dhidi ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda akipinga maombi yake ya kufanya marejeo ya uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro. 
 
Sheikh Ponda anakabiliwa na kesi ya jinai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, akidaiwa kufanya uchochezi maeneo mbalimbali mkoani humo na kukaidi amri ya Mahakama ya Kisutu ya Mei 9, mwaka jana ya kumtaka kuhubiri amani kwa jamii likiwa ni sharti la kifungo cha mwaka mmoja nje.
 
Awali, Sheikh Ponda aliomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro imfutie shtaka hilo la kukaidi amri ya Mahakama ya Kisutu, lakini Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro ilimkatalia, aliamua kuwasilisha maombi Mahakama Kuu akiiomba ifanye marejeo ya uamuzi huo.
 
Hata hivyo, maombi hayo yalitupiliwa mbali Desemba 11, mwaka jana baada ya DPP kumwekea pingamizi kuwa hati ya kiapo iliyokuwa ikiunga mkono maombi yake, ilikuwa na kasoro za kisheria kwa kuwa haikuwa ikitimiza matakwa ya Sheria ya Viapo kwa kutokuonyesha jina la aliyeapa na tarehe.
 
Baada ya kutupiliwa mbali, Wakili wa Sheikh Ponda, Juma Nassoro aliwasilisha tena maombi hayo.
 
mahakamani hapo baaada ya kufanya marekebisho ya kasoro hizo za kisheria.

0 comments:

Post a Comment