Friday, February 28, 2014

6:16 AM


Ugonjwa wa homa ya nguruwe umelipuka tena mkoani Mbeya na kuua zaidi ya nguruwe 900 katika wilaya za Mbeya na Rungwe.
Mganga Mkuu wa Mifugo Mkoani Mbeya, Solomon Nong’ona akizungumza nasi jana alisema, ugonjwa huo umerudi tena baada ya kuzuka kwa mara ya kwanza Januari mwaka huu na kutokomezwa.
Alisema kufuatia kuzuka tena kwa ugonjwa huo, serikali kupitia sekta ya mifugo imepeleka dawa mkoani humo ambazo zinasaidia kupunguza kasi ya kuenea.
Nong’ona  alisema kufuatia kuzuka kwa ugonjwa huo wananchi nao wanajitahidi kununua dawa hizo ili kuudhibiti na kuwakinga nguruwe wanaowafuga.

0 comments:

Post a Comment