Tuesday, February 25, 2014

7:37 AM

Msanii Ray C

Staa Nguli wa muziki wa Bongo Fleva,Rehema Chalamila’Ray C’ambaye pia aliwahi kutumia madawa ya kulevya na kuacha amefungua asasi iitwayo Ray C Foundation iliyoanzishwa rasmi February 2014,ofisi ipo Jengo la Biashara Complex,Mwananyamala,Dar.Ray C kupitia account yake instagram aliandika kuwa nia na madhumuni ya asasi hiyo ni kuelimisha vijana na jamii yote kwa ujumla madhara ya utumiaji wa madawa ya kulevya kwani madawa ya kulevya ni tatizo kubwa sana lililoikumba nchi yetu ya Tanzania.

Msanii Ray C  Pia aliongeza kuwa katika jamii kulikuwepo na ukimya mkubwa juu ya haya madawa ya kulevya,majadiliano juu ya ulevi wa madawa hayo yalikuwa hayazungumziki kwa uwazi hata kidogo japo madhara ya matumizi ya dawa za kulevya ni makubwa sana na yanatisha katika jamii yetu hapa Tanzania

Msanii Ray Afunguka

Ameongeza kuwa nia na madhumuni ya kuanzisha Ray C Foundation hasa ni kuhamasisha na kuelimisha vijana na jamii nzima athari za utumiaji madawa ya kulevya na kuwafikia walengwa ndani ya jamii na katika maeneo ya nchi nzima!!!!!!Eeh Mungu Tuepushe na Janga hili Nguvu kazi ya Taifa isipotee………We need your Support…Alimalizia

0 comments:

Post a Comment