Monday, March 31, 2014

3:17 PM


Jose Chameleone amenyang’anywa gari yake aina ya Escalade na maofisa wa URA baada ya mamlaka hiyo kudai kwamba msanii huyo ameshindwa kulipa kodi yenye thamani ya shilingi milioni saba ya Uganda.
Muda mchache kabla ya kuanza kwa onyesho kubwa la Tubonge la msanii huyo, maofisa wa URA waliikamata gari yake hiyo ya kifahari.
Kwa mujibu wa mtandao wa Redpapper wa nchini Uganda,msanii huyo alijaribu kuwakatalia wasikuchukue gari lake akidai atakufa na mtu atakayeichukua lakini kauli hiyo haikufua dafu kwa mamlaka hiyo. “Hii ni gari yangu binafsi na nina haki yake, mtu yeyote akigusa Escalade yangu, nami tufe pamoja naye,” alidai Chameleone.
CHAMELEONHata hivyo Chameleone alidai kuwa hana tatizo lolote kulipa kodi lakini mamlaka hiyo haikutolea vigezo walivyotumia kupata jumla ya shilingi milioni 7 za Uganda ambazo ndizo pesa wanazomdai

0 comments:

Post a Comment